Kwa mujibu wa taarifa zilizo naswa
toka kwa wafanyakazi wa Meli hiyo ambao hawakutoa ushirikiano
kuzungumza na waandishi wa habari, zilizonaswa wakati wakilaumiana
zimeleeza kuwa mafundi wa kampuni hiyo walikuwa wakichomelea katika moja
ya vyumba vya chini vya Meli hiyo ndipo cheche za moto zilipopenya na
kuangukia katika sehemu ya pili ya kuhifadhia mizigo na kuanza kuwaka.
Sehemu hiyo ya mizigo kulikuwa kumehifadhiwa shehena ya magodoro pamoja
na mito ya makochi tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda mjini Bukoba
Mkoani Kagera leo usiku.
Ni
hali halisi ndani ya Sehemu hiyo ya mizigo kulikuwa kumehifadhiwa
magodoro pamoja na mito ya makochi tayari kwa ajili ya kusafirishwa
kwenda mjini Bukoba Mkoani Kagera leo usiku.Maafisa wa kikosi hicho walijitosa kuhakikisha moto huo hausambai katika maeneo mengine ya Meli ya Mv Victoria ambapo walifanikiwa kuuzima huku ukiwa tayari umeteketeza magodoro yote pamoja na mito ya makochi iliyokuwa katika chumba cha kuhifadhia mizigo.
No comments:
Post a Comment