Wednesday, December 26, 2012

HII NDIYO POMBE INAYOUWA WATU UGANDA.


Polisi nchini Uganda wameanza msako wa watengenezaji wa pombe ya kienyeji aina ya gin, iliyosababisha vifo vya watu wanne na kuwasababishia upofu wengine wawili ndani ya wiki mbili.Polisi wamesema watu hao walikufa baada ya kunywa pombe hiyo kwenye baa inayomilikiwa na watengenezaji pombe kwenye makazi duni ya vitongoji vya Katanga, Kikumikikumi karibu na Makerere na kitongoji cha Sir Apollo Kaggwa Jijini Kampla.

Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Wandegeya, Ceasar Tusingwire amesema wanadhani kuwa watu hao walikufa baada ya kunywa pombe hiyo iliyokuwa imefungwa kwenye vifungashio vya mifuko ya plastiki na kwenye madumu.

Kufuatia tukio hilo polisi nchini Uganda imewaonya wananchi kutopendelea kunywa pombe za kienyeji kutokana na nyingi kuwa na dalili za sumu.

No comments:

Post a Comment