Uchunguzi uliofanywa na mtandao huu umebaini kuwa siku hizi watu wanaolewa au kuoa ili kuifurahisha jamii tu.
Ndoa
zetu zimejaa usaliti wa kila hali.Chanzo cha maovu hayo ni tamaa ya
pesa, kutoridhika kimapenzi, ushawishi wa kupandishwa kazi na mambo
mengine kibao
=> USHAURI WANGU KWA WANAWAKE....
Kama mtu ana akili nzuri naamini atakuwa ni mwerevu. Nawasihi wanawake muache tabia ya AIBU.Muulize kinachomsibu mumeo.
Kama unaogopa kumwambia basi unaweza kumwanzisha tu pole pole wakati wa mnafanya mapenzi. Mwambie leo nataka unishike hapa. Leo tujaribu staili hii, napenda ukifanya hivi, usiwe unakuja mapema...Dear uko bize mno, naomba uwe unanijali na tufanye mara kwa mara...
Kama unaogopa kumwambia basi unaweza kumwanzisha tu pole pole wakati wa mnafanya mapenzi. Mwambie leo nataka unishike hapa. Leo tujaribu staili hii, napenda ukifanya hivi, usiwe unakuja mapema...Dear uko bize mno, naomba uwe unanijali na tufanye mara kwa mara...
Wanaume ni kama watoto wadogo na
ukiwa mjanja unaweza kumbadilisha unavyotaka hasa katika mambo ya
mapenzi...Vinginevyo utakuwa ni mtu wa kuibiwa kila leo.
Hata huko nje utapata mume wa mtu. Mwanzoni mambo yatakuwa moto lakini baadaye mtazoeana na mambo yatakuwa yale yale.
Halafu kama ni mume wa mtu na anafanya nje ya ndoa , unajuaje kama hana mnyororo wa wanawake huko nje?. Mmoja tu akiwa na UKIMWI kwenye huo mnyororo basi kila memba wa huo mnyororo anaishia kuudaka....
=> USHAURI WANGU KWA WANAUME:...
Ni jambo la busara sana kumjali mkeo.Wanaume wengine mnajitakia wenyewe.Unakuta mwanaume yuko busy masaa 24 yote.....
Hajui nyumbani wamekula nini, kurudi kwake ni usiku, tena akiwa amelewa.
Akiulizwa alikuwa wapi ,ugomvi unaanza.Akipewa
penzi, basi ni bao moja tu, hoi.Unategemea huyu mwanamke akimpata
wa kumbembeleza huko nje atamkataa kweli?.....Mfanye mkeo ajivunie
kuwa na wewe.
Inashangaza sana kuona kuwa mwanaume yuko tayari apate lunch na secretary wake, lakini kwa mkewe anakuwa bahiri......
Jamani, wapendeni wake zenu. Tenga
muda wa kutosha ku enjoy na mkeo.....Na wakati wa tendo la ndoa,
usikurupuke.Mwandae vizuri mkeo na hakikisha unamfikisha kileleni
****************
=> Narudia tena kwenu mliooa.
Hakikisheni kuwa wake zenu wanaridhika kimapenzi. Vinginevyo ni
matatizo tupu. Nitafurahi sana kama mtakuwa amesikia ushauri wangu. Na
wengine toeni ushauri wenu jamani ili tuiokoe ndoa zetu....
=>>JAMANI, VYOMBO VYAHABARI VIMEELISHA VYA KUTOSHA. NI WAKATI WETU KUBADILIKA SASA.....
EPUKA KUJICHAFUA KATIKA MAGAZETI. HESHIMU NDOA YAKO.
No comments:
Post a Comment