Monday, January 14, 2013

RAPPER DNA APIGA MARUFUKU NYIMBO ZAKE KUTUMIKA KWENYE KAMPENI ZA SIASA .



DNA
Rapper DNA Kutoka Grandpa Records Kenya Amesema hata kubali Chama chochote au Mwanasiasa nchini Kenya Atumie wimbo wake wowote katika kampeni za Siasa bila ruhusa na maelekezo maalum kutoka record lebel yake ya Grandpa. DNA ambaye ameshawahi kuipeleke Banki fulani mahakamani kwa sababu za kubadilisha wimbo wake wa Banjuka Ukawa Benkika amesema vyama vya siasa hupenda sana kubadilisha au kutumia nyimbo za wasanii bila ruhusa zao. DNA alikaririwa na sammisago.com akisema hajafunga milango kwa wale wanaotaka kutumia Melody au wimbo wa Maswali ya Polisi kwenye kampeni ila awe tayari kufata maelekezo na makubaliano ya Record lebel hio.
Pia kuhusu vigezo vya chama ,DNA amesema chama atakacho kipa wimbo wake lazima kiwe ni chama kilicho saidia vijana na wananchi wa Kenya. Hataki wimbo wake uhusike kwenye chama kisicho tekeleza sera na ahadi zake.

No comments:

Post a Comment