Friday, January 18, 2013

AFYA YA MANUMBA BADO NI TETE

Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya The Aga Khan, Jaffer Dharsee, amesema hali ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba (pichani), sio nzuri na bado anahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi. Dk. Dharsee alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa alikuwa na malaria kali iliyosababisha kulazwa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) na yuko huko hadi sasa akiwa katika uangalizi  wa katibu wa madaktari. 

Msemaji wa familia ya Manumba, James Kilaba, alisema hali ya ndugu yao inaleta matumaini tofauti na ilivyokuwa awali na zaidi wanawasikiliza madaktari kwa sababu ndio wanaojua hali yake.
Kilaba aliwaomba Watanzania kumuombea ndugu yao ili apone na kuendelea kutimiza wajibu wa kulitumikia Taifa.
Viongozi mbalimbali wa Serikali, akiwano Rais Jakaya Kikwete jana walifika hospitali hapo kumjilia hali Kamishna Manumba.
Wengine  ni Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete; Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Saidi Mwema na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment